Pages - Menu

Thursday, January 11, 2018

HISTORIA ZA MATAJIRI WAKUBWA DUNIANI WALIOWEKEZA KATIKA BITCOIN NA SARAFU ZA KIDIJITALI KWA UJUMLA.


WINK LEVOSS




Mapacha hawa walizaliwa mnamo tarehe 21 mwezi August 1981, wajasiliamali wakubwa wa biashara za internet (internet). Umaarufu wao ulianza mwaka 2014 mara baada ya kumshitaki Mark Zuckerberg (mmiliki wa mtandao wa kijamii wa facebook) madai ya kuwa aliiba wazo lao la mtandao wa kijamii unaounganisha watu. Walishinda kesi hiyo na kulipwa takribani dola milion 65 za kimarekani (takribani sh 139,750,000,000/= za kitanzania).


Mapacha hao Cameron na Tyler winklevoss walitumia fedha hizo kuwekeza katika bitcoin. Walikiambia kituo cha habari cha CNBC kwa kuwa walijiingiza katika bitcoin na kuanza kuifatilia tangu mwaka 2012 wakati bitcoin ikiwa na thamani ya dola za kimarekani 10(takribani 22,400/= za kitanzania)
Hadi kufikia leo utajiri wao umeongezeka ma kufikia dola bilioni 1.3

WINK LEVOSS MAPACHA MABILIONEA WA KWANZA WA BITCOIN


BILL GATES

Huyu ni mwanzilishi wa Shirika la Microsoft, Mfanyabiashara wa kiamerika na mwekezaji mkubwa. Hadi kufikia January mwaka 2018 utajiri wake umeongezeka na kufikia dola za kimarekani bilion 91.1 kutoka dola za kimarekani bilioni 84.4 mwaka 2014 alipowekeza katika bitcoin. Billgate aliwekeza asilimia 0.5 tu ya utajiri wake wa wakati huo. Billgate amesikika mara nyingi akisema “Njia halisi ya kuwa bilionea bila kuwa na asilimia kubwa za kupoteza mtaji wakoni kuchunguza dunia inapoelekea na kufika huko wa kwanza kwa kuwekeza”
Mwaka 2014 alikiambia kituo cha BLOOMBERG kuwa Bitcoin ni zaidi ya sarafu na inaleta mvuto zaidi na ushawishi kuitumia katika mahamisho makubwa ya kifedha”
Utafiti unasema kwamba kama WINKLEVOSS BROTHERS wanamiliki zaidi ya Bitcoin 100,000 ni rahisi kwa mtu kama Billgate kumiliki chache zaidi ya hizo. Ukilinganisha thamani ya bitcoin 100,000 ilikuwa ni sawa na dola za kimarekani milioni 45, hiyo ilikuwa ni chini ya asilimia 0.5 ya utajiri wa Billgate kwa wakati huo. Alisikika akisema kuwa Bitcoin bado ipo hatua za mwanzo sana na ni rahisi kumfanya mtu yoyote trilionea.


MARK ZUCKERBERG

Alizaliwa mnamo tarehe 14 May mwaka 1984, ni mtaalamu wa kutengeneza program za kompyuta na mjasiliamali mkubwa wa biashara za kimtandao. Hadi kufikia Nov mwaka 2017 alikuwa akikadiliwa kuwa na utajiri wa dola za kimarekani milion 74.2

Taarifa zilizotoka January 5 mwaka huu zinasema Mark Zuckerberg ameweka wazi kuhusu mpango wake kwenye mabadiliko haya ya kiteknolojia na alishaanza rasmi kuangalia jinsi ya kufanya uwekezaji zaidi katika teknolojia hii ya sarafu za kidigitali kama bitcoin wakati akiongea na kituo cha habari cha CNBC. Hadi sasa yupo kwenye hatua za kuifahamu kiundani.



FINMAN

Alipokuwa na miaka 15 aliwaomba sana wazazi wake kuwa angependa aachane na shule sababu ya mwalim mmoja aliyekuwa akimsumbua college. Alianza kumchukia mwalimu huyo baada ya kumkaripia kwa kumwambia kuwa hakuwa kitu ni bora aachane na shule na akaajiliwe katika kiwanda cha kuoka mikate na keki cha Mc Donalds. Ndipo Finman alipoamua kuweka DAU na wazazi wake kuwa endapo atafikisha miaka 18 akiwa milionea basi wasingemlazimisha tena kuendelea na shule. Alisikika pia akisema katika kituo kimoja cha habari kuwa “Naushukuru uwekezaji wangu wa utani na hasira katika bitcoin, sitalazimishwa tena kuendelea na masomo”.
Hadi sasa Finmani anamiliki takribani bitcoin 403 ambazo zina thamani ya kila moja na kuufikisha utajiri wake kiasi cha dola za kimarekani milioni 1. Amewekeza pia katika sarafu nyingine za kidigitali kama litecoin na Etheleum.
Finman alisema “Siku njema zitaendelea kuja na thamani ya sarafu za kidijitali tukizishuhudia zikipanda hadi mara 1000 zaidi ya zilivyo sasa”
Finman alianza kwa kuwekeza dola 1000 (takribani 2,240,000/=) mwaka 2011 alipokuwa na miaka 12, zawadi aliyopewa na bibi yake na kaka yake Scott.


JEREMY GARDNER

Kijana mwenye umri wa miaka 24 anaesemekana kuwa kijana mwenye bahati sana kuwahi kutokea baada ya kuwekeza katika bitcoin.
Mnamo mwaka 2013 rafiki yake alimpa zawadi ya bitcoin ili wabadilishane kwa fedha ndogo sana. Alizoea kuona watu wakiitumia kununulia vitu vidogo sana kama pizza wakati huo.
Ilipofika mwaka 2017 Gardner alipatwa na bumbuwazi wakati akiwa matembezini nchinin afrika ya kusini. Aliingia mtandaoni baada ya kusikia fununu na kukuta thamani ya bitcoin moja kupanda na kufikia dola za kimarekani 2400 (takribani 40,057,243/=). Anaitabili bei ya bitcoin kuendellea kupanda zaidi na kufikia kiasi cha kuweza kumilikiwa na watu wachache sana kwaajili ya kununulia vitu vyenye thamani kubwa sana na pengine vya kifahari na thamani maradufu ya vilivyopo sasa kama magari na majumba ya kifahari.
Umaarufu wake umezidi kuongezeka baada ya kuanza kuishi maisha ya kitajiri na tabia yake ya kupenda kuwanunulia wafanyakazi wenzake chakula wanapokuwa mikutanoni. Hupenda pia kuchangia utajiri wake alioupata kutoka katika uwekezaji wa bitcoin na wengine. Anamiliki kampuni nyingine kubwa ya fedha za kidigitali iitwayo AUGUR.

Friji ya Jeremy Gardner iliyopo kwake yenye nembo mbalimbali za sarafu za kidigitali.


PIZZA STORY
Mnamo mwaka 2010 nchini FROLIDA mtaalam wa program LASZ HANYECZ alibembeleza kuuziwa pizza 2 kwa bitcoin 10,000 alizokuwa ametengeneza kupitia komputa ya nyumbani.
“Ilionekana bei ya bicoin ingeshuka zaidi kwa siku za usoni hivyo niliona halikuwa wazo baya kubadilishana na pizza”
Thamani ya bitcoin 10,000 kwa sasa ni zaidi ya 400,572,430,000/= za kitanzania, na ndivyo jina la utani la bitcoin lifahamikalo kama “pizza coin” yaani sarafu pizza  lilivyopatikana.

Matukio ya watu wakijutia kuhusu kuhisi kupoteza bahati zao adimu yameendelea kutokea ambapo mwaka 2017 tweet moja iliyotumwa katika mtandao wa kijamii wa tweeter tarehe 16 mwezi Mei mwaka 2011, ilionesha mtu mmoja alietumia jina la GREG SCHOEN akijutia kwa kuuza bitcoin zake 1,700 kwa bei ya dola za kimarekani 0.3 (takribani 672/=) alizonunua kwa bei ya dola za kimarekani 0.6 (takribani 1,344/= za kitanzania kila moja) na baadae kupanda na kufikia dola za kimarekani 8 (takriban 17,920/= za kitanzania kila moja) kwa kila sarafu. Hakika anajutia mara nyingi zaidi kwa sasa ambapo leo hii angekuwa na utajiri wa zaidi ya 68,097,313,100/= za kitanzania endapo angezitunza kwa miaka 6 tu.



Hizo ni baadhi ya story tu zinazovutia kuihusu teknolojia hii inayoonekana kuwa changamoto kubwa na muujiza kwa watu wengi, mengi yanazidi kutokea yakiwemo majuto na kubadili maisha ya wengi. Post ijayo tutaongelea hatua zilizochukuliwa na nchi za afrika katika kuendana na mabadiliko haya ya kiteknolojia.

No comments:

Post a Comment