Kufuatiwa kuwepo kwa tetesi zinazosema kuwa serikali
ya China imepanga kuzifungia kampuni zote zinazofanya biashara ya sarafu
digitali nchini humo mara baada ya mwaka jana benki kuu ya nchi hiyo kuanzisha
vikwazo juu ya kampuni zinazojishughulisha na uchimbaji wa sarafu digitali,, na
ilianza kwa kutunga sheria ngumu zinazolenga kuzibana kampuni hizi.
Sheria hizi zilipelekea kampuni baadhi kufungwa kama
RENMIMBI iliyokuwa ikifanya biashara zake nchini humo na nyingine kuanza
kujiandaa kuhama kutafuta makao yake nchi nyingine.
Siku za hivi karibuni mwanzilishi na msimamizi mkuu
wa kampuni ya BTCC ambae pia amejipatia ubilionea mkubwa kutokana na kufanya
biashara hii ametabiri kuwa nchi nyingi kama China zitaonyesha kupinga
teknolojia hii lakini mwishoni zitalazimika kukubali na kuendana nayo .
”Hamna mwananchi atakaelazimishwa kutumia kitu asichokipenda angali kizuri na bora zaidi kipo” BOBBY LEE alisikika akikiambia kituo cha habari cha CNN.
Ikiwa ni siku chache mara baada ya kauli ya Bobby
Lee kutangazwa na vyombo vya habari hatimae serikali ya China imesikika pia
ikisema haipangi kuikataa na kuitokomeza teknolojia hii bali kuichunguza na
kuidhibiti kwa njia chanya dhidi ya matumizi makubwa ya nishati yanayotumika
katika uchimbaji wa sarafu hizo.
Mmiliki wa kampuni nyingine ya uchimbaji wa bitcoin
nchini humo (schwani) amesema mamlaka za kiserikali za nchi hiyo zimeagiza
wachimbaji wote wa sarafu hizi kuwakilisha anwani zao pamoja na kiasi cha
bitcoin wanazochimba kila siku. Sio huyo tu lakini pia mmiliki wa kampuni ya
BITMAIN Wu Jihan alikiambia kituo cha habari cha Bishijie kuwa uchimbaji wa
sarafu digitali kama bitcoin na matumizi yake kukua nchini humo zinaisaidia
sana serikali ya nchi hiyo kuendelea hivyo sio rahisi kuitelekeza,
Kinachotakiwa ni kutafuta njia mbadala dhidi ya matumizi makubwa ya nishati
yanayotumika.
Nini maoni yako juu ya utabiri wa Bilionea Bobby Lee?

No comments:
Post a Comment