Pages - Menu

Wednesday, January 10, 2018

HISTORIA YA BITCOIN NA FEDHA DIGITALI KWA UJUMLA

Mnamo january 3 2009 bitcoin(sarafu digitali) ya kwanza iligunduliwa na mtaalamu wa kuunda programu mbalimbali za kompyuta na masuala ya kiuchumi aitwae SATOSHI NAKAMOTO.
Kabla Satoshi Nakamoto kutoweka kusikojulikana aliweka utambulisho wake wazi akijitaja kama raia wa wa japani mwenye umri wa takribani miaka 37. Utambulisho unaonekana kuwa sio sahihi kulingana na uwezo wake wa kuandika lugha ya kingereza kwa ufasaha na katika kuunda program iliyotumika kutengeneza bitcoin na tovuti ya bitcoin.org


Aliendelea kusaidiana na kundi lake hadi katikati ya mwaka 2010 ambapo alikabidhi kila kitu kwa GAVIN ANDRESEN (mwanzilishi wa 3D graphics na mtaalam wa programu za virtual reality) baada ya kukamilisha zoezi zima la uundaji wa bitcoin.
Hadi sasa hamna ukweli halisia unaomtambulisha Satoshi Nakamoto japokuwa yapo makisio mbalimbali yaliyopatikana kumuhusu mtafiti ma mtaalamu huyu aliyeleta mapinduzi makubwa katika sekta ya fedha na teknolojia duniani kote.
Yapo makisio yanayosema haikuwa mtu mmoja bali kundi la watu wenye dhamira moja, lakini pia ukweli huu sio halisia kwa sababu ya kukosa vithibitisho kamili.


Bitcoin kwa lugha rahisi tunaitafsiri kama sarafu digitali inatengenezwa kwa mchakato uitwao mining na kumbukumbu zake huifadhiwa kwenye mfumo maalumu uitwao blockchain ambao pia hutumika katika uhamishaji wa bitcoin kutoka kwa mtumaji X kwenda kwa mpokeaji Y bila kuwepo kwa mamlaka yoyote ya kifedha katikati,.
Neno Mining katika utengenezwaji wa bitcoin halina maana ya uchimbaji wa madini kama ilivyozoeleka bali lina maana ya mchakato wa kutatua mantiki za kihesabu kwa kutumia program maalum za kompyuta.Mara baada ya mchakato huo kukamilika makundi ya bitcoin yanayopatikana(block) huwekwa katika mfuatano/mlolongo maalumu(chain) kulingana na jinsi yalivyopatikana na ndio maana hutambulika kama blockchain.
Kadri bitcoin zinavyotengenezwa ndivyo mfuatano/mlolongo huu huongezeka urefu na ugumu pia katika utatuzi wa mantiki za kihesabu pia huongezeka. Hii imepelekea thamani yake kihesabu kupanda lakini pia gharama za uhamishaji(transaction fee). Changamoto hii imeweza kutatuliwa na baadhi ya sarafu digitali nyingine zilizovumbuliwa baada ya bitcoin ni kama Ethereum.


MAENDELEO YA BITCOIN TANGU KUUNDWA KWAKE.
Japokuwa sekta nyingi za kifedha duniani zimeonyesha kuvutiwa na mapinduzi haya ya kiteknolojia bado zina mashaka kuhusu utekelezaji wa utumiaji wa sarafu za aina hii. Mnamo mwaka 2014 tulishuhudia benki kuu ya Australia ikifunga akanti zote zilizotumika katika ununuaji au uuzaji wa bitcoin.Kati ya miaka ya 2013 na 2014 mamlaka kuu ya benki za ulaya na mamlaka ya udhibiti wa taasisi za kifedha nchini humo zikitoa tahadhari kuhusu hatari iliyopo katika uwekezaji wa sarafu hii ya bitcoin uliokuwa ukiendelea.
Ndani ya mwaka huo wa 2013 pia Forbes ilitaja uwekezaji katika bitcoin kama uwekezaji bora wa mwaka huo wakati ilipofika 2014 kituo kikubwa cha habari cha Blomberg kiliutaja uwekezaji katika bitcoin kama uwekezaji mbaya kuliko uwekezaji wowote duniani.
Ilipofika 2015 meza ya habari ya kituo cha Blomberg ilishuhudia kufunikwa kwa habari zilizohusu bitcoin tu katika upande wa habari za kifedha na kiuchumi kwa ujumla.
Kwa mujibu wa bitincharts.com (tovuti inayoonyesha ukuaji wa bitcoin) hadi kufikia mwaka 2017 kulikuwa na bitcoin wallet(mifuko maalumu ya kimtandao inayotumika kuhifadhi bitcoin) ipatayo 9,272 yenye bitcoin zenye thamani zaidi ya dola za kimarekani million 1.
Wapo pia mabepari kama Peter Thiel ambao waliwekeza zaidi ya dola za kimarekani milioni 3 ili kusaidia miradi na sekta mbalimbali zilizohusika na maendeleo ya sarafu hii.
VIDEO IKIELEZEA NAMNA BITCOIN INAVYOWEZA KUONDOA UMASIKINI DUNIANI.







ASILI YA BITCOIN KUWA NA BEI TETE.
Mnamo mwaka 2011 bei ya bitcoin ilikua ghafla na kufikia dola 30 za kimarekani (takribani 67,200/=). Badae katikati ya mwaka 2013  na 2014 tarehe 10 mwezi aprili bei ya bitcoin ilikua zaidi na kufikia dola 266 za kimarekani (takribani 595,840/=) kabla ya kuanguka tena thamani yake hadi dola za kimarekani 50(takribani 112,000/=)
Hadi kufikia mwezi august mwaka 2014 bei ya bitcoin ilikuwa chini ya dolla 600$(1,344,000/=).Kulingana na maelezo ya gwiji wa mambo ya kiuchumi Mark T Wiliam, bitcoin ina hali ya kuwa na bei tete mara 7 zaidi ya bei ya dhahabu.
Ndani ya mwaka 2013 waandisi wa habari, wanachumi na benki kuu ya Estonia walipaza sauti wakiitaja sarafu ya bitcoin kama mpango wa kimtandao ulioundwa ili kutapeli watu na haikuwa biashara wala sarafu halisi. Mwanasheria profesa wa sheria katika chuo cha chikago alisimama kuthibithisha kuwa bitcoin haikuonekana kuwa mpango danganyifu sababu hakipo ata kimoja kilchosemwa kuhusu bitcoin ambacho kilionekana kuwa uongo, watu waliweza kuimiliki katika mifuko yao ya kimtandao, kuuza na kununua bila taasisi zozote za kifedha za kati kuhusika, bei pia ilipanda na kushuka kulingana na mahitaji yake, yote hayo yalikuwa halisi, yalioonekana na haikuwa udanganyifu.
Mwishoni wa mwaka 2014 benki kuu ya dunia ilithibitisha na kuhitimisha kuwa bitcoin haikuwa mpango danganyifu bali kitu halisia. Sio benki kuu ya dunia tu, Shirikisho la balaza la fedha la uswisi lilihitimisha pia kwa kusema bitcoin haikuwa mpango danganyifu sababu kulikuwa hamna faida yoyote iliyohaidiwa katika uwekezaji wake bali makisio ya mtu binafsi na kupenda kujihusisha katika uwekezaji wake.

Adi mwezi julai mwaka 2017 sekta na taasisi nyingi za kifedha dunia tayari zilikuwa zimeikubali bitcoin kama sarafu halisia na sio mpango danganyifu isipokuwa baadhi ya watu binafsi maarufu kama bilionea na mwekezaji maarufu aitwae Howard Marks ambae bado aliendelea kuitaja bitcoin kama mpango danganyifu. Tarehe 12 mwezi Septemba, Jamie Dimon (Mmoja kati ya watendaji wakuu wachache sana duniani kuwa mabilionea) ambae alikuwa akitumikia kama mkurugenzi mtendaji wa moja kati ya benki kubwa duniani inayotajwa kuwa ya sita kwa kumiliki mali zenye thamani kubwa duniani iitwayo JP Morgan Chase, aliitaja bitcoin kama udanganyifu wa kimtandao na alitoa onyo kali katika kampuni yake kwa yoyote ambae angejihusisha na biashara ya bitcoin angepoteza kazi yake. Zero Hedge (tovuti inayotoa habari za kiuchumi) ilitoa fununu kuwa wakati Howard Dimon akitoa onyo hilo JP Morgan mwenyewe alitajwa akinunua bitcoin kwaajili ya wateja wake. Tarehe 9 mwezi january 2018 Jamie Dimon ameonekana akiongea na shirika la habari la CNN akisema anajutia kuiita biashara hii ya bitcoin kama biashara danganyifu ambapo thamani ya bitcoin moja imefikia kiasi cha kuuzwa takribani dola za kimarekani 14,398 (kati ya 35,521,281/=  na 46,461,909/=)

Kutokana na ongezeko la bei ya bitcoin siku hadi siku mabilionea wengi sana ambao walinunua wakati ikiwa chini wameendelea kuonekana kona nyingi za dunia.
                          ………………………….

Tutaendelea katika post ijayo kuwataja mabilionea ambao wamebadilisha kazi zao na kujikita katika biashara hii ya sarafu za kidigitali, benki za nchi mbali mbali ambazo zimeikubali bitcoin na matarajio makubwa yaliyopo yaliyopo katika sarafu hizi kwa wawekezaji wake. Ahsante!!

No comments:

Post a Comment