Pages - Menu

Thursday, January 11, 2018

HATUA ZILIZOCHUKULIWA HADI SASA NA NCHI ZA AFRIKA KUHUSU SARAFU HIZI HASA BITCOIN.


KENYA NA AFRIKA YA MASHARIKI
Kenya ilijulikana kupitia Bitpesa (Tovutia inayoweza mteja kubadili bitcoin kuwa fedha na fedha kwa bitcoin) ambayo imesaidia nchi za afrika ya mashariki kuitumia sarafu ya bitcoin kwa
kasi zaidi.
Lakini pia mtandao wa mawasiliano wa M-PESA mwaka 2017 ulisikika ukisema 
“tunaona fursa kubwa ndani ya bitcoin na teknolojia hii mpya".

NIGERIA
Hii ni kati ya nchi zenye idadi kubwa ya watu barani Afrika na inachukuliwa kama nchi mojawapo inayoikubali na kuitumia bitcoin kwa kiasi kikubwa. Haikuwa maajabu ilipofika oktoba 2016 Bitx (Tovuti inayojishughulisha na uhifadhi wa bitcoin) ilipofikisha mipakuo(downloads) takribani 100,000 kutoka nchini humo pekee.Ilipofika mwezi Julai mwaka 2017 kiasi cha fedha iliyopo kwenye mzunguko LocalBitcoin (Tovuti nyingine inayosaidia uuzaji na ununuaji wa bitcoin) ilipofika dola za kimarekani milion 3, na kati ya hizo asilimia 32 ilikuwa ikitoka nchini Nigeria.
Benki kuu ya Nigeria imeendelea kusema bado inafatilia njia chanya  ya kuendana na mabadiliko haya ya kiteknolojia.

AFRIKA KUSINI
Mfuko wa kuhifadhi bitcoin wa BITX adi kufikia 2017 ilikuwa imefikisha asilimia 66 ya watumiaji kutoka Afrika kusini, wakati 23 kati ya hao walikuwa wakiitumia sarafu hii kwenye uhamishaji wa fedha wa haraka, na asilimia 40 wakiitumia kama sehemu ya uwekezaji. Lakini pia hadi sasa Afrika kusini ni kati ya nchi zinazomiliki ATM ya huduma za BITCOIN.

GHANA NA AFRIKA YA MAGHARIBI
Tovuti ya Ghana Dot Com imesaidia sana katika kuifanikisha teknolojia hii kufika mbali baada ya kuanzisha mchakato wa kutengeneza bitcoin nchini humo chini ya uongozi wa profesa NII NARKU QUAVOUR, ambapo kwa hesabu inachangia asilimia 3 ya ada zote kwenye mfumo wa blockchain (blockchain fees).
Tovuti nyiingine ijulikanayo kwa jina la KITIWA, Mwezi Juni ilifikisha takribani dola za kimarekani 40000 kutokana na kuunganishwa na kampuni nyingine ya mawasiliano na  simu za mkononi KITIWA ilionyesha kufikia viwango vya juu zaidi vya ubora katika kuendeleza huduma hii.


ZIMBABWE
Ilipofika mwaka 2017,Bitcoin ilivunja rekodi kwa mara ya kwanza duniani kote kwa kufikisha bei ya dola za kimarekani 2000 (takriban 4,800,000/=) nchini ZIMBABWE. Baada ya benki nyingi za ZIMBABWE kukumbwa na vikwazo vingi kutokana na migogoro ya kisisasa uliyokuwa ikiendelea nchini humo.

Ziliona teknolojia ya bitcoin kama njia mbadala na fursa pekee ya kuziendeleza kutokana na asili ya bitcoin ya kutofungamana na sekta za kifedha za kiserikali.
Shukrani kwa LocalBitcoin (Tovuti ya kuuzia na kununulia bitcoin iliyopo nchini zimbabwe) iliyosaidia sana biashara hii, ambayo ilishuhudia ongezeko kubwa la watu kutoka zimbabwe na kuifanya kufungua matawi mawili zaidi yafahamikayo kama BitMari na BitFinance.
Sio hivyo tu, watu wameendelea kuiamini bitcoin hadi kufikia kuitumia kwenye matumizi ya kawaida kabisa kama vile kutolea mahari, inaweza kuwa kitu cha ajabu lakin kijana mmoja afahamikaye kwa jina la ANTONY MBURU alionesha kuiamini zaidi sarafu hii na kuitumia kulipia mahali mara baada ya kuongezeka zaidi ya mara 10 tangu alipozinunua, kituo cha habari cha NTV kilimuonyeha akisema.

Matukio mengi kuihusu bitcoin yameendelea kutokea nchini humo siku hadi siku.

Nchi nyingine ambazo wananchi wake wametajwa wakionyesha kushiriki sana katika biashara hii ni Uganda na Tanzania, Nchi ya SENEGAL imetoa kauli rasmi ya kuanza kuitumia teknolojia hii mwishoni mwa mwaka huu na kuisambaza kupitia WESTERN AFRICA AND MONETARY UNION.

No comments:

Post a Comment