Sheria iliyopitishwa tarehe 1 January mwaka huu nchini Gibraltar inayozitaka kampuni zote zinazojihusisha na sarafu digitali hasa Bitcoin kuwa na leseni maalum za kiserikali kutoka mamlaka ya GFSC (Gibraltar Financial Service Commission).
![]() |
| The chief Minister of Gibraltar Hon. Fabian Picardo |
Sheria hii inazitaka kampuni hizo kuboresha
njia za mawasiliano kati yao na wateja na kutunga sheria binafsi za kila
kampuni zinazolenga kulinda masilahi ya fedha zinazowekwa na wananchi katika
biashara hiyo,sheria hizo zitapitiwa na mamlaka hiyo kwa umakini kabla ya
kutumika.
Mwezi December mwaka jana bunge la nchi hiyo
liliadhimia na kuweka wazi lengo lake la
kuhakikisha Gibraltar inakuwa nchi pekee yenye mvuto wa uwekezaji katika
biashara hiyo na utumiaji mzuri wa teknolojia hii.
Serikali
ya nchi hiyo hadi sasa inaonyesha kwa kiwango kikubwa kuiamini teknolojia hii
mpya ya sarafu za kigeni na kuitumia kama njia ya kurudisha uchumi wake katika
hali ya kawaida Mara ya baada ya uchumi wao kuyumbishwa na kuharibika kwa
British naval dockyard (bandari kubwa iliyokuwa ikitegemewa na nchi ya
Gibraltar.)

No comments:
Post a Comment