Pages - Menu

Saturday, January 13, 2018

ADA ZA KUHAMISHA BITCOIN KUPUNGUA

Baada ya kushuhudia gharama za mahamisho ya bitcoin yakipanda kwenye robo ya mwisho mwaka 2017, hatimaye zimeanza kushuka kwa mara nyingine. Leo tovuti ya Bitcoinfee.com imeonyesha wastani wa dola 15 kwa kila mahamisho ya bitcoin yaliyofanywa duniani.



Tovuti za kubadilisha bitcoin kama bitfinex, wiki hii imetangaza pia kutakuwa na kupungua kwa kiasi kikukwa kwa gharama za kutoa bitcoin kutoka kwa watumiaji wa tovuti hii.

Japokuwa wastani wa gharama za mahamisho ya bitcoin ya dola 14 mpaka dola 16 bado kuonekana zipo juu ila haya ni maendeleo makubwa ukilinganisha na wastani wa dola 30 iliyokuepo mwaka jana mwezi December.

Masaa machache yaliyopita tovuti nyingine za localbitcoin pamoja na BTC.com  zimeongeza teknolojia ya segwit inayolenga kupunguza gharama za mahamisho ya bitcoin na hiyo imeshuhudiwa na watumiaji wake wengi baada ya gharama kupungua. BTC.com iliongeza kwa kuandika katika   blog yake kuwa
"watumiaji wake watafurahia huduma yake kutokana na kushuka kwa gharama. Hii imetokana na teknolojia ya segwit kuongezwa katika mifumo yake ya mifuko ya kuhifadhia bitcoin kwa watumiaji wote wa simu za mkononi na kompuya''.
Hadi sasa ni asilimia 11 pekee ya kampuni zinazojishughulisha na bitcoin zilizoikubali teknolojia ya segwit yenye lengo la kupunguza gharama, pengine matokeo haya ya kupungua kwa gharama za uhamishaji wa bitcoin yanayoendelea kuoneshwa na kampuni zinazoitumia teknolojia hiyo zitapelekea kampuni nyingi kuitumia.

Unahisi nini athari na faida za kuitumia teknolojia hii katika matumizi ya bitcoin? toa maoni yako katika nafasi ya comments iliyopo chini.

No comments:

Post a Comment